Ayubu 13:1-5
1
“Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
2
Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
3
Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
4
Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
5
Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
Settings