Skip to content
Ayubu 13:6-12

Ayubu 13:6-12

6
Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
7
Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
8
Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
9
Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
10
Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
11
Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
12
Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options