Rukia maudhui
Mwanzo 45:25-28

Yakobo Asikia Habari na Kufufuka Moyo

Mwanzo 45:25-28
25
Basi wakatoka Misri na kufika kwa baba yao Yakobo katika nchi ya Kanaani.
26
Wakamwambia baba yao, “Yosefu angali hai! Ukweli ni kwamba yeye ndiye mtawala wa Misri yote.” Yakobo akapigwa na bumbuazi; hakuwasadiki.
27
Lakini walipokwisha kumweleza kila kitu ambacho Yosefu alikuwa amewaambia, na alipoona magari ya kukokotwa Yosefu aliyokuwa amempelekea ya kumchukua aende Misri, roho ya baba yao Yakobo ikahuishwa.
28
Ndipo Israeli akasema, “Nimesadiki! Mwanangu Yosefu bado yu hai. Nitakwenda nikamwone kabla sijafa.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options