Rukia maudhui
Mwanzo 22:15-19

Agano lithibitishwa kwa kiapo

Mwanzo 22:15-19
15
Basi malaika wa Bwana akamwita Abrahamu kutoka mbinguni mara ya pili,
16
akasema, “Ninaapa kwa nafsi yangu, asema Bwana, kwamba kwa sababu umefanya jambo hili na hukunizuilia mwanao, mwana wako wa pekee,
17
hakika nitakubariki, na nitauzidisha uzao wako kama nyota za angani na kama mchanga ulioko pwani. Wazao wako watamiliki miji ya adui zao,
18
na kupitia uzao wako mataifa yote duniani yatabarikiwa, kwa sababu umenitii.”
19
Ndipo Abrahamu akawarudia watumishi wake, wakaondoka wakaenda wote pamoja mpaka Beer-Sheba. Abrahamu akaishi huko Beer-Sheba.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options