Rukia maudhui
Wagalatia 5:1-6

Simameni Imara Katika Uhuru wa Kikristo

Wagalatia 5:1-6
1
Kristo alitupa uhuru, akataka tubaki huru. Hivyo simameni imara wala msikubali tena kulemewa na kongwa la utumwa.
2
Sikilizeni! Mimi, Paulo, nawaambieni kwamba kama mkikubali kutahiriwa, basi Kristo hatawafaidia chochote.
3
Namshuhudia tena kila mtu anayekubali kutahiriwa kwamba inampasa kushika sheria yote.
4
Ninyi mnaotafuta kuhesabiwa haki kwa njia ya sheria mmetengwa na Kristo, mko mbali na neema ya Mungu.
5
Kwa maana, kwa njia ya Roho kwa imani, tunangojea kwa shauku tumaini la haki.
6
Kwa maana ndani ya Kristo Yesu, kutahiriwa au kutokutahiriwa hakuleti tofauti, bali lililo muhimu ni imani itendayo kazi kwa njia ya upendo.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options