Wagalatia 5:7-12
7
Mlikuwa mkipiga mbio vizuri. Ni nani aliyewazuia msiitii kweli?
8
Ushawishi wa namna hiyo haukutokana na yule anayewaita.
9
“Chachu kidogo huchachua donge zima.”
10
Nina hakika katika Bwana kwamba hamtakuwa na msimamo mwingine. Mtu anayewachanganya anastahili adhabu, hata awe nani.
11
Lakini ndugu zangu, kama mimi bado ninahubiri kuhusu kutahiriwa, kwa nini bado ninateswa? Katika hiyo hali basi, kwazo la msalaba limeondolewa.
12
Laiti hao wanaowavuruga wangejihasi wao wenyewe!
Settings