Rukia maudhui
Amosi 5:21-27

Mungu Anakataa Ibada Isiyo na Maana

Amosi 5:21-27
21
“Ninachukia, ninazidharau sikukuu zenu za dini; siwezi kuvumilia makusanyiko yenu.
22
Hata ingawa mnaniletea sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka za nafaka, sitazikubali. Ingawa mnaniletea sadaka nzuri za amani, sitazitambua.
23
Niondoleeni kelele za nyimbo zenu! Sitasikiliza sauti za vinubi vyenu.
24
Lakini acheni haki itiririke kama mto, na uadilifu uwe kama kijito kisichokauka!
25
“Je, mliniletea dhabihu na sadaka kwa miaka arobaini kule jangwani, ee nyumba ya Israeli?
26
Mmeyainua madhabahu ya mfalme wenu, Sikuthi mungu wenu mtawala, na Kiuni mungu wenu wa nyota, ambao mliwatengeneza wenyewe.
27
Kwa sababu hiyo nitawapeleka uhamishoni mbali kupita Dameski,” asema Bwana, ambaye jina lake ni Mungu Mwenye Nguvu Zote.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options