Amosi 5:21-24
21
“Ninachukia, ninazidharau sikukuu zenu za dini; siwezi kuvumilia makusanyiko yenu.
22
Hata ingawa mnaniletea sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka za nafaka, sitazikubali. Ingawa mnaniletea sadaka nzuri za amani, sitazitambua.
23
Niondoleeni kelele za nyimbo zenu! Sitasikiliza sauti za vinubi vyenu.
24
Lakini acheni haki itiririke kama mto, na uadilifu uwe kama kijito kisichokauka!
Settings