2 Nyakati 11:5-12
5
Rehoboamu akaishi Yerusalemu akajenga miji yenye ngome katika Yuda:
6
Akajenga Bethlehemu, Etamu, Tekoa,
7
Beth-Suri, Soko, Adulamu,
8
Gathi, Maresha, Zifu,
9
Adoraimu, Lakishi, Azeka,
10
Sora, Aiyaloni na Hebroni. Hii ndiyo iliyokuwa miji iliyojengewa ngome katika Yuda na Benyamini.
11
Akaimarisha ulinzi wake na kuweka majemadari ndani yake, pamoja na ghala za mahitaji ya vyakula, mafuta ya zeituni na divai.
12
Akaweka ngao na mikuki katika miji na kuifanya iwe imara sana. Kwa hiyo Yuda na Benyamini zikawa zake.
Settings