Rukia maudhui
1 Samweli 19:11-14

1 Samweli 19:11-14

11
Sauli akatuma watu nyumbani mwa Daudi wailinde hiyo nyumba na kumuua asubuhi. Lakini Mikali, mkewe Daudi, akamwonya akisema, “Kama hukukimbia kuokoa maisha yako usiku huu, kesho yake utauawa.”
12
Basi Mikali akamteremsha Daudi kupitia dirishani, naye akakimbia na kuokoka.
13
Kisha Mikali akachukua kinyago, akakilaza kitandani, akakifunika kwa vazi na kukiwekea singa za mbuzi kichwani.
14
Sauli alipotuma watu kumkamata Daudi, Mikali akasema, “Yeye ni mgonjwa.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options