1 Wakorintho 16:5-9
5
Baada ya kupitia Makedonia nitakuja kwenu, maana ninakusudia kupitia Makedonia.
6
Huenda nitakaa nanyi kwa muda, au hata kukaa nanyi kipindi chote cha baridi, ili mweze kunisaidia katika safari yangu, popote niendapo.
7
Kwa maana sitaki niwaone sasa na kupita tu; natarajia kuwa nanyi kwa muda wa kutosha, kama Bwana akipenda.
8
Lakini nitakaa Efeso mpaka wakati wa Pentekoste,
9
kwa maana mlango mkubwa umefunguliwa kwangu kufanya kazi yenye matunda, nako huko kuna adui wengi wanaonipinga.
Settings