Skip to content
1 Wakorintho 16:1-4

Mchango kwa Watakatifu wa Yerusalemu

1 Wakorintho 16:1-4
1
Basi kuhusu changizo kwa ajili ya watakatifu: Kama nilivyoyaagiza makanisa ya Galatia, fanyeni vivyo hivyo.
2
Siku ya kwanza ya kila juma, kila mmoja wenu atenge kiasi cha fedha, kulingana na mapato yake na fedha hizo aziweke akiba, ili nitakapokuja pasiwe na lazima ya kufanya mchango.
3
Kwa hiyo nitakapowasili, nitawapa wale mtakaowachagua barua za kuwatambulisha, ili kuwatuma wapeleke zawadi zenu huko Yerusalemu.
4
Kama ikionekana ni vyema na mimi niende, basi hao watu watafuatana nami.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options