- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Zaburi7
Listen to this chapter
0:00
0:00
Sala ya kuomba wokovu na kumtumaini Mungu
1
Ombolezo la Daudi kwa Bwana kwa sababu ya Kushi, Mbenyamini. Ee Bwana, Mungu wangu, ninakukimbilia wewe, uniokoe na kunikomboa na wote wanaonifuatia,
2
la sivyo watanirarua kama simba na kunichana vipande vipande, asiwepo wa kuniokoa.
Kiapo cha Daudi cha kutokuwa na hatia
3
Ee Bwana, Mungu wangu, kama nimetenda haya na kuna hatia mikononi mwangu,
4
au ikiwa nimemtenda uovu aliye na amani nami, au nimemnyangʼanya adui yangu pasipo sababu,
5
basi adui anifuatie na kunipata, auponde uhai wangu ardhini na kunilaza mavumbini.
Kumwomba Mungu ainuke kuwa mwamuzi
6
Amka kwa hasira yako, Ee Bwana, inuka dhidi ya ghadhabu ya adui zangu. Amka, Mungu wangu, uamue haki.
7
Kusanyiko la watu na likuzunguke. Watawale kutoka juu.
8
Bwana na awahukumu kabila za watu. Nihukumu Ee Bwana, kwa kadiri ya haki yangu, kwa kadiri ya uadilifu wangu, Ewe Uliye Juu Sana.
9
Ee Mungu mwenye haki, uchunguzaye mawazo na mioyo, komesha ghasia za waovu na ufanye wenye haki waishi kwa amani.
10
Ngao langu ni Mungu Aliye Juu Sana, awaokoaye wanyofu wa moyo.
Uhakika wa Hukumu ya Mungu
11
Mungu ni mwamuzi mwenye haki, Mungu aghadhibikaye kila siku.
12
Kama hakutuhurumia, atanoa upanga wake, ataupinda na kuufunga uzi upinde wake.
13
Ameandaa silaha zake kali, ameweka tayari mishale yake ya moto.
14
Yeye aliye na mimba ya uovu na achukuaye mimba ya ghasia huzaa uongo.
15
Yeye achimbaye shimo na kulifukua hutumbukia katika shimo alilochimba mwenyewe.
16
Ghasia azianzishazo humrudia mwenyewe, ukatili wake humrudia kichwani.
Nadhiri ya Shukrani
17
Nitamshukuru Bwana kwa ajili ya haki yake, na nitaliimbia sifa jina la Bwana Aliye Juu Sana.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Reading Width chars
Options
Study Note