Rukia maudhui

Zaburi149

Wito wa Sifa za Furaha

1
Msifuni Bwana. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.
2
Israeli na washangilie katika Muumba wao, watu wa Sayuni na wafurahi katika Mfalme wao.
3
Na walisifu jina lake kwa kucheza na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
4
Kwa maana Bwana anapendezwa na watu wake, anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.
5
Watakatifu washangilie katika heshima hii, na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.

Watakatifu Watekeleza Hukumu ya Mungu

6
Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,
7
ili walipize mataifa kisasi na adhabu juu ya mataifa,
8
wawafunge wafalme wao kwa minyororo, wakuu wao kwa pingu za chuma,
9
ili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao. Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote. Msifuni Bwana.
Use arrow keys to navigate
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options