- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Zaburi139
Listen to this chapter
0:00
0:00
Mungu Anajua Yote
1
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, umenichunguza na kunijua.
2
Unajua ninapoketi na ninapoinuka; unatambua mawazo yangu tokea mbali.
3
Unafahamu kutoka kwangu na kulala kwangu; unaelewa njia zangu zote.
4
Kabla neno halijafika katika ulimi wangu, wewe walijua kikamilifu, Ee Bwana.
5
Umenizunguka nyuma na mbele; umeweka mkono wako juu yangu.
6
Maarifa haya ni ya ajabu mno kwangu, ni ya juu sana kwangu kuyafikia.
Hakuna Kutoroka Uwepo wa Mungu
7
Niende wapi nijiepushe na Roho yako? Niende wapi niukimbie uso wako?
8
Kama nikienda juu mbinguni, wewe uko huko; nikifanya vilindi kuwa kitanda changu, wewe uko huko.
9
Kama nikipanda juu ya mbawa za mapambazuko, kama nikikaa pande za mbali za bahari,
10
hata huko mkono wako utaniongoza, mkono wako wa kuume utanishika kwa uthabiti.
11
Kama nikisema, “Hakika giza litanificha na nuru inayonizunguka iwe usiku,”
12
hata giza halitakuwa giza kwako, usiku utangʼaa kama mchana, kwa kuwa giza ni kama nuru kwako.
Nimeumbwa kwa Kicho na kwa Ajabu
13
Kwa maana wewe ndiwe uliyeumba utu wangu wa ndani; uliniunga pamoja tumboni mwa mama yangu.
14
Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa kwa namna ya ajabu na ya kutisha; kazi zako ni za ajabu, ninajua hayo kikamilifu.
15
Umbile langu halikufichika kwako, nilipoumbwa mahali pa siri. Nilipoungwa pamoja kwa ustadi katika vilindi vya nchi,
16
macho yako yaliniona kabla mwili wangu haujakamilika. Siku zangu zote ulizonipangia ziliandikwa katika kitabu chako kabla haijakuwepo hata moja.
17
Tazama jinsi yalivyo ya thamani mawazo yako kwangu, Ee Mungu! Jinsi jumla yake ilivyo kubwa!
18
Kama ningezihesabu, zingekuwa nyingi kuliko mchanga. Niamkapo, bado niko pamoja nawe.
Ombi Juu ya Waovu na Kujichunguza
19
Laiti ungewachinja waovu, Ee Mungu! Ondokeni kwangu, ninyi wamwaga damu!
20
Wanazungumza juu yako wakiwa na kusudi baya, adui zako wanatumia vibaya jina lako.
21
Ee Bwana, je, nisiwachukie wanaokuchukia? Nisiwachukie sana wanaoinuka dhidi yako?
22
Sina kitu zaidi ya chuki dhidi yao, ninawahesabu ni adui zangu.
Unichunguze, Ee Mungu
23
Ee Mungu, nichunguze, uujue moyo wangu, nijaribu na ujue mawazo yangu.
24
Uone kama kuna njia iletayo machukizo ndani yangu, uniongoze katika njia ya milele.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Reading Width chars
Options
Study Note