Rukia maudhui

Zaburi120

Kilio cha Kuomba Wokovu

1
Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
2
Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.

Hatima ya Wadanganyifu

3
Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
4
Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.

Kuomboleza Uhamishoni Kati ya Watu Wenye Uadui

5
Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
6
Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
7
Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.
Use arrow keys to navigate
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options