Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Altars: For incense

6 mistari · 31 vipengele

Mistari kuhusu For incense

  1. “Tengeneza madhabahu kwa mbao za mshita kwa ajili ya kufukizia uvumba.

  2. Madhabahu hayo yawe mraba, urefu na upana wake dhiraa moja, na kimo cha dhiraa mbili, nazo pembe zake zitakuwa kitu kimoja nayo.

  3. Funika hayo madhabahu juu na pande zote na pia pembe zake kwa dhahabu safi, na uifanyizie ukingo wa dhahabu kuizunguka.

  4. Tengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili ya madhabahu chini ya huo ukingo, ziwe mbili kila upande, za kushikilia hiyo mipiko itumikayo kuibebea madhabahu.

  5. Tengeneza mipiko kwa miti ya mshita na uifunike kwa dhahabu.

  6. Weka hayo madhabahu mbele ya lile pazia lililo mbele ya Sanduku la Ushuhuda, lililo mbele ya kiti cha rehema kilicho juu ya Sanduku la Ushuhuda, mahali ambapo nitakutana nawe.