Skip to content
Zaburi 81:6-10

Zaburi 81:6-10

6
Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
7
Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
8
“Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
9
Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
10
Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 90 chars

Options