8
“Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
9
Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
10
Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.