Zaburi 81:11-16
11
“Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
12
Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
13
“Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
14
ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
15
Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
16
Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”
Settings