Skip to content
Zaburi 81:1-5

Zaburi 81:1-5

1
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
2
Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
3
Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
4
hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
5
Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options