Skip to content
Zaburi 78:40-51

Zaburi 78:40-51

40
Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
41
Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
42
Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
43
siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
44
Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
45
Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
46
Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
47
Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
48
Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
49
Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
50
Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
51
Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options