Skip to content
Zaburi 78:12-29

Zaburi 78:12-29

12
Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
13
Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
14
Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
15
Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
16
alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
17
Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
18
Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
19
Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
20
Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
21
Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
22
kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
23
Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
24
akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
25
Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
26
Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
27
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
28
Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
29
Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options