Zaburi 78:12-16
12
Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
13
Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
14
Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
15
Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
16
alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
Settings