Zaburi 77:2-9
2
Nilipokuwa katika taabu, nilimtafuta Bwana, usiku nilinyoosha mikono bila kuchoka na nafsi yangu ilikataa kufarijika.
3
Ee Mungu, nilikukumbuka wewe, nikalia kwa huzuni; nikatafakari, roho yangu ikadhoofika.
4
Ulizuia macho yangu kufumba; nilikuwa nasumbuka, nikashindwa kusema.
5
Nilitafakari juu ya siku zilizopita, miaka mingi iliyopita,
6
nilikumbuka nilivyoimba nyimbo usiku. Moyo wangu ulitafakari na roho yangu ikauliza:
7
“Je, Bwana atakataa milele? Je, hatatenda mema tena?
8
Je, upendo wake usio na mwisho umetoweka milele? Je, ahadi yake imekoma nyakati zote?
9
Je, Mungu amesahau kuwa na huruma? Je, katika hasira amezuia huruma yake?”
Settings