Zaburi 66:8-20
8
Enyi mataifa, msifuni Mungu wetu, sauti ya sifa yake isikike,
9
ameyahifadhi maisha yetu na kuizuia miguu yetu kuteleza.
10
Ee Mungu, wewe ulitujaribu, ukatusafisha kama fedha.
11
Umetuingiza kwenye nyavu na umetubebesha mizigo mizito migongoni mwetu.
12
Uliwaruhusu watu watukalie vichwani, tulipita kwenye moto na kwenye maji, lakini ulituleta kwenye nchi iliyojaa utajiri tele.
13
Nitakuja hekaluni mwako na sadaka za kuteketezwa na kukutimizia nadhiri zangu:
14
nadhiri ambazo midomo yangu iliahidi na nilizotamka kwa kinywa changu nilipokuwa katika shida.
15
Nitakutolea dhabihu za wanyama wanono na sadaka za kondoo dume, nitakutolea mafahali na mbuzi.
16
Njooni msikilize ninyi nyote mnaomcha Mungu, nami niwaambie aliyonitendea.
17
Nilimlilia kwa kinywa changu, sifa zake zilikuwa katika ulimi wangu.
18
Kama ningekuwa nimeyaficha maovu moyoni mwangu, Bwana asingekuwa amenisikiliza;
19
lakini hakika Mungu amenisikiliza na amesikia sauti yangu katika maombi.
20
Sifa apewe Mungu, ambaye hakulikataa ombi langu wala kunizuilia upendo wake!
Settings