Zaburi 66:8-12
8
Enyi mataifa, msifuni Mungu wetu, sauti ya sifa yake isikike,
9
ameyahifadhi maisha yetu na kuizuia miguu yetu kuteleza.
10
Ee Mungu, wewe ulitujaribu, ukatusafisha kama fedha.
11
Umetuingiza kwenye nyavu na umetubebesha mizigo mizito migongoni mwetu.
12
Uliwaruhusu watu watukalie vichwani, tulipita kwenye moto na kwenye maji, lakini ulituleta kwenye nchi iliyojaa utajiri tele.
Settings