Zaburi 50:9-14
9
Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
10
Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
11
Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
12
Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
13
Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
14
Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
Settings