Skip to content
Zaburi 50:16-21

Zaburi 50:16-21

16
Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
17
Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
18
Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
19
Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
20
Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
21
Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options