Skip to content
Zaburi 50:7-13

Zaburi 50:7-13

7
“Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
8
Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
9
Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
10
Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
11
Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
12
Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
13
Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options