Skip to content
Zaburi 49:6-12

Zaburi 49:6-12

6
wale wanaotegemea mali zao na kujivunia utajiri wao mwingi?
7
Hakuna mwanadamu awaye yote awezaye kuukomboa uhai wa mwingine, au kumpa Mungu fidia kwa ajili yake.
8
Fidia ya uhai ni gharama kubwa, hakuna malipo yoyote yanayotosha,
9
ili kwamba aishi milele na asione uharibifu.
10
Wote wanaona kwamba watu wenye hekima hufa; wajinga na wapumbavu vivyo hivyo huangamia na kuwaachia wengine mali zao.
11
Makaburi yao yatabaki kuwa nyumba zao za milele, makao yao vizazi vyote; ingawa walikuwa na mashamba na kuyaita kwa majina yao.
12
Lakini mwanadamu, licha ya utajiri wake, hadumu; anafanana na mnyama aangamiaye.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options