Zaburi 41:4-9
4
Nilisema, “Ee Bwana nihurumie, niponye, maana nimekutenda dhambi wewe.”
5
Adui zangu wanasema kwa hila, “Lini atakufa, na jina lake litokomee kabisa.”
6
Kila anapokuja mtu kunitazama, huzungumza uongo, huku moyo wake hukusanya masingizio; kisha huondoka na kuyasambaza huku na huko.
7
Adui zangu wote hunongʼonezana dhidi yangu, hao huniwazia mabaya sana, wakisema,
8
“Ugonjwa mbaya sana umempata, kamwe hatainuka tena kitandani mwake.”
9
Hata rafiki yangu wa karibu niliyemwamini, yule aliyekula chakula changu ameniinulia kisigino chake.
Settings