Skip to content
Zaburi 40:13-17

Zaburi 40:13-17

13
Ee Bwana, uwe radhi kuniokoa; Ee Bwana, njoo hima unisaidie.
14
Wote wanaotafuta kuuondoa uhai wangu, waaibishwe na kufadhaishwa; wote wanaotamani kuangamizwa kwangu, warudishwe nyuma kwa aibu.
15
Wale waniambiao, “Aha! Aha!” wafadhaishwe na iwe aibu yao.
16
Lakini wote wakutafutao washangilie na kukufurahia, wale wapendao wokovu wako siku zote waseme, “Bwana atukuzwe!”
17
Lakini bado mimi ni maskini na mhitaji; Bwana na anifikirie. Wewe ndiwe msaada wangu na Mwokozi wangu; Ee Mungu wangu, usikawie.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options