Zaburi 35:7-16
7
Kwa vile walinifichia wavu wao bila sababu, na bila sababu wamenichimbia shimo,
8
maafa na yawapate ghafula: wavu walionifichia na uwatege wenyewe, na waanguke katika shimo hilo, kwa maangamizo yao.
9
Ndipo nafsi yangu itashangilia katika Bwana na kuufurahia wokovu wake.
10
Nitapaza sauti yangu nikisema, “Ni nani aliye kama wewe, Ee Bwana? Wewe huwaokoa maskini kutokana na wale walio na nguvu kuliko wao, maskini na mhitaji kutokana na wanaowanyangʼanya!”
11
Mashahidi wakatili wanainuka, wananiuliza mambo nisiyoyajua.
12
Wananilipa baya kwa jema na kuiacha nafsi yangu ukiwa.
13
Lakini walipokuwa wagonjwa, nilivaa nguo ya gunia na nikajinyenyekesha kwa kufunga. Maombi yangu yaliponirudia bila kujibiwa,
14
niliendelea kuomboleza kama vile wao ni rafiki au ndugu. Niliinamisha kichwa chini kwa huzuni kama ninayemwombolezea mama yangu.
15
Lakini nilipojikwaa, walikusanyika kwa shangwe; washambuliaji walijikusanya dhidi yangu bila mimi kujua. Walinisingizia pasipo kukoma.
16
Kama watu wasiomcha Mungu, wamenidhihaki, wamenisagia meno.
Settings