Skip to content
Zaburi 35:11-18

Zaburi 35:11-18

11
Mashahidi wakatili wanainuka, wananiuliza mambo nisiyoyajua.
12
Wananilipa baya kwa jema na kuiacha nafsi yangu ukiwa.
13
Lakini walipokuwa wagonjwa, nilivaa nguo ya gunia na nikajinyenyekesha kwa kufunga. Maombi yangu yaliponirudia bila kujibiwa,
14
niliendelea kuomboleza kama vile wao ni rafiki au ndugu. Niliinamisha kichwa chini kwa huzuni kama ninayemwombolezea mama yangu.
15
Lakini nilipojikwaa, walikusanyika kwa shangwe; washambuliaji walijikusanya dhidi yangu bila mimi kujua. Walinisingizia pasipo kukoma.
16
Kama watu wasiomcha Mungu, wamenidhihaki, wamenisagia meno.
17
Ee Bwana, utatazama mpaka lini? Niokoe maisha yangu na maangamizi yao, uhai wangu wa thamani kutokana na simba hawa.
18
Nami nitakushukuru mbele ya kusanyiko kubwa, nitakusifu katikati ya watu wengi.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options