Zaburi 18:7-11
7
Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya milima ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
8
Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
9
Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
10
Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
11
Alifanya giza kuwa kitu chake cha kujifunika, hema lake kumzunguka, mawingu meusi ya mvua ya angani.
Settings