4
Kamba za mauti zilinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
5
Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili.
6
Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu anisaidie. Kutoka hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika mbele zake, masikioni mwake.