Skip to content
Zaburi 18:7-19

Zaburi 18:7-19

7
Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya milima ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
8
Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
9
Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
10
Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
11
Alifanya giza kuwa kitu chake cha kujifunika, hema lake kumzunguka, mawingu meusi ya mvua ya angani.
12
Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
13
Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
14
Aliipiga mishale yake na kutawanya adui, naam, umeme mwingi wa radi na kuwafukuza.
15
Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwako, Ee Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwako.
16
Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
17
Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
18
Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
19
Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options