Rukia maudhui
Zaburi 119:89-96

LAMEDI: Neno la Mungu Ni la Milele na Imara

Zaburi 119:89-96
89
Ee Bwana, neno lako ni la milele, linasimama imara mbinguni.
90
Uaminifu wako unaendelea kwa vizazi vyote, umeiumba dunia, nayo inadumu.
91
Sheria zako zinadumu hadi leo, kwa kuwa vitu vyote vinakutumikia.
92
Kama nisingefurahia sheria yako, ningeangamia katika taabu zangu.
93
Sitasahau mausia yako kamwe, kwa maana kwayo umehifadhi maisha yangu.
94
Uniokoe, kwa maana mimi ni wako, kwa kuwa nimetafuta mausia yako.
95
Waovu wanangojea kuniangamiza, bali mimi ninatafakari sheria zako.
96
Katika ukamilifu wote ninaona mna kikomo, lakini amri zako hazina mpaka.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options