Zaburi 119:97-104
97
Aha! Tazama, sheria yako naipenda mno ajabu. Ninaitafakari mchana kutwa.
98
Amri zako zimenipa hekima zaidi kuliko adui zangu, kwa kuwa nimezishika daima.
99
Nina akili zaidi kuliko walimu wangu wote, kwa kuwa ninatafakari juu ya sheria zako.
100
Nina ufahamu zaidi kuliko wazee, kwa kuwa ninayatii mausia yako.
101
Nimezuia miguu yangu isiende kwenye kila njia mbaya, ili niweze kutii neno lako.
102
Sijaziacha sheria zako, kwa kuwa umenifundisha wewe mwenyewe.
103
Tazama jinsi maneno yako yalivyo matamu kwangu, matamu kuliko asali katika kinywa changu!
104
Ninapata ufahamu kutoka mausia yako, kwa hiyo ninachukia kila njia ya upotovu.
Settings