Skip to content
Zaburi 119:105-112

Zaburi 119:105-112

105
Neno lako ni taa ya miguu yangu na mwanga katika njia yangu.
106
Nimeapa na nimethibitisha, kwamba nitafuata sheria zako za haki.
107
Nimeteseka sana, uhifadhi maisha yangu, Ee Bwana, sawasawa na neno lako.
108
Ee Bwana, pokea sifa za hiari za kinywa changu, nifundishe sheria zako.
109
Ingawa maisha yangu yako hatarini siku zote, sitasahau sheria yako.
110
Waovu wamenitegea mtego, lakini sijayakiuka maagizo yako.
111
Sheria zako ni urithi wangu milele, naam ni furaha ya moyo wangu.
112
Nimekusudia moyoni mwangu kuyafuata maagizo yako mpaka mwisho.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options