Zaburi 119:81-88
81
Nafsi yangu inazimia kwa kutamani wokovu wako, lakini nimeweka tumaini langu katika neno lako.
82
Macho yangu yamefifia, nikingoja ahadi yako; ninasema, “Utanifajiri lini?”
83
Ingawa nimekuwa kama kiriba kwenye moshi, bado sijasahau maagizo yako.
84
Mtumishi wako itampasa angoje mpaka lini? Ni lini utawaadhibu washtaki wangu?
85
Wenye majivuno wananichimbia mashimo, kinyume na sheria yako.
86
Amri zako zote ni za kuaminika; unisaidie, kwa sababu watu wananishtaki bila sababu.
87
Walikaribia kabisa kunifuta kutoka uso wa dunia, lakini sijaacha mausia yako.
88
Yahifadhi maisha yangu sawasawa na upendo wako, nami nitatii sheria za kinywa chako.
Settings