Skip to content
Zaburi 119:73-80

Zaburi 119:73-80

73
Mikono yako ilinifanya na kuniumba, nipe ufahamu niweze kujifunza amri zako.
74
Wakuchao wafurahie wanaponiona, kwa kuwa nimeweka tumaini langu katika neno lako.
75
Ee Bwana, ninajua kwamba sheria zako ni za haki, katika uaminifu wako umeniadhibu.
76
Upendo wako usiokoma uwe faraja yangu, sawasawa na ahadi yako kwa mtumishi wako.
77
Huruma yako na inijie ili nipate kuishi, kwa kuwa naifurahia sheria yako.
78
Wenye majivuno na waaibishwe kwa kunikosea mimi bila sababu, lakini mimi nitatafakari juu ya mausia yako.
79
Wale wakuchao na wanigeukie mimi, hao ambao wanazielewa sheria zako.
80
Moyo wangu usiwe na lawama katika kutii maagizo yako, ili nisiaibishwe.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options