Zaburi 119:65-72
65
Mtendee wema mtumishi wako Ee Bwana, sawasawa na neno lako.
66
Nifundishe maarifa na uamuzi mzuri, kwa kuwa ninaamini amri zako.
67
Kabla sijapata shida nilipotea njia, lakini sasa ninalitii neno lako.
68
Wewe ni mwema, unalotenda ni jema, nifundishe maagizo yako.
69
Ingawa wenye majivuno wamenisingizia uongo, nitafuata mausia yako kwa moyo wangu wote.
70
Mioyo yao ni katili na migumu, bali mimi napendezwa na sheria yako.
71
Ilikuwa vyema mimi kupata shida ili nipate kujifunza maagizo yako.
72
Sheria inayotoka kinywani mwako ina thamani kubwa kwangu kuliko maelfu ya vipande vya fedha na dhahabu.
Settings