Rukia maudhui
Zaburi 119:57-64

HETHI: Mungu Ndiye Fungu Langu na Azimio Langu

Zaburi 119:57-64
57
Ee Bwana, wewe ni fungu langu, nimeahidi kuyatii maneno yako.
58
Nimetafuta uso wako kwa moyo wangu wote, nihurumie sawasawa na ahadi yako.
59
Nimezifikiri njia zangu na nimeelekeza hatua zangu katika mausia yako.
60
Nitafanya haraka bila kuchelewa kuzitii amri zako.
61
Hata waovu wanifunge kwa kamba, sitasahau sheria yako.
62
Usiku wa manane ninaamka kukushukuru kwa sababu ya sheria zako za haki.
63
Mimi ni rafiki kwa wale wote wakuchao, kwa wote wanaofuata mausia yako.
64
Ee Bwana, dunia imejaa upendo wako, nifundishe maagizo yako.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options