Rukia maudhui
Zaburi 106:1-5

Utangulizi: Wito wa Sifa na Sala

Zaburi 106:1-5
1
Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
2
Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
3
Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
4
Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
5
ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options