Zaburi 105:37-45
37
Akawatoa Israeli katika nchi wakiwa na fedha na dhahabu nyingi, wala hakuna hata mmoja kutoka kabila zao aliyejikwaa.
38
Misri ilifurahi walipoondoka, kwa sababu hofu ya Israeli ilikuwa imewaangukia.
39
Alitandaza wingu kama kifuniko, na moto kuwamulikia usiku.
40
Waliomba, naye akawaletea kware, akawashibisha kwa mkate wa mbinguni.
41
Alipasua mwamba, maji yakabubujika, yakatiririka jangwani kama mto.
42
Kwa maana alikumbuka ahadi yake takatifu, aliyompa Abrahamu mtumishi wake.
43
Aliwatoa watu wake kwa furaha, wateule wake kwa kelele za shangwe,
44
akawapa nchi za mataifa, wakawa warithi wa mali wengine walikuwa wameitaabikia:
45
alifanya haya ili wayashike mausia yake na kuzitii sheria zake. Msifuni Bwana.
Settings