Rukia maudhui
Zaburi 104:24-30

Zaburi 104:24-30

24
Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
25
Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
26
Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
27
Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
28
Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
29
Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
30
Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options