Zaburi 104:19-23
19
Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
20
Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
21
Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
22
Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
23
Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
Settings