Zaburi 104:10-18
10
Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
11
Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
12
Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
13
Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
14
Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
15
divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
16
Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
17
Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
18
Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
Settings